vimarsana.com

Page 362 - Carousel Constructor Plugins News Today : Breaking News, Live Updates & Top Stories | Vimarsana

Azam FC Wakataa Kumuachia Dube

Azam FC Wakataa Kumuachia Dube Azam FC Wakataa Kumuachia Dube UONGOZI wa Azam FC, umesema kuwa hawapo tayari kumuuza staa wao, Mzimbabwe, Prince Dube, kwenda Simba na badala yake ataendelea kubaki kikosini kwao.   Hiyo ikiwa ni siku chache tangu ziwepo tetesi za Simba kuwa kwenye mipango ya kumnasa mshambuliaji huyo anayeongoza kwa mabao Ligi Kuu Bara akiwa amepachika 12.   Taarifa zilizopo kwa sasa ni kwamba, hivi karibuni mshambuliaji huyo ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Azam, hivyo atakuwa hapo hadi 2024.Akizungumza na Spoti Xtra,Mtendaji Mkuu wa Azam, Abdulkarim Amin ‘Popat’ alisema Dube hataenda timu yoyote hapa nchini, bali atabaki Azam.

Brian Simba Afungasha Virago Lebo ya Vanessa Mdee

  Rapa aliyekuwa anamilikiwa na rekodi lebo ya Mdee Music chini ya msanii Vanessa Mdee aitwaye Brian Simba, amesema amemaliza mkataba wa kusimamiwa na lebo hiyo na hivi sasa yupo huru kufanya kazi zake mwenyewe. Brian Simba amesema anamshukuru sana Vanessa Mdee kufanya nae kazo kwani amempa uzoefu mpya kwenye upande wa muziki pia amemfanya kuzunguka mikoa na nchi mbalimbali. Masomo hayajanirudisha nyuma yamenipa exposure mpya kwenye maisha, kufanya kazi na Vanessa Mdee ilinisaidia vitu vingi kama kuzunguka mikoa na nchi mbalimbali, ilikuwa experience nzuri ila mkataba wetu wa kufanya kazi uliisha amesema Brian Simba  Pia amezungumzia kuhusu ujio wa Album yake mpya na uwepo wa wasanii wengine wapya wanaofanya muziki wa HipHop  kwa kusema  Album yangu itatoka mwezi wa nane ina ngoma nyingi sana na kali, hapo katikati nilipokuwa shule walikuja marapa wengi wakali ila ni marafiki zangu wote, napenda wakali tuwe wengi .

Wahuni Waiba Kengele ya Kanisa Yenye Kilo 500

  WATU wasiojulikana wameripotiwa kuiba kengele ya kanisa la Virgin Mary Orthodox lililoko eneo la Limuru kaunti ya Kiambu nchini Kenya ambapo tayari maafisa wa polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo. Kulingana na Katibu wa kanisa la Virgin Mary Ordhodox James Warari alisema genge la wezi lilivamia kanisa hilo Alhamisi, Aprili 22,2021 na kuiba kengele hiyo ambayo inasemekana kuwa na uzito wa kilogramu 500. “Kisa hicho kilitokea Alhamisi Usiku, tuliamka asubuhi na tukagundua kwamba kengele hiyo haikuwepo. Mtu mmoja hawezi akabeba kengele hiyo kwa sababu ni nzito sana. Tunajua kulikuwa na watu kadhaa walishirikiana kubeba,” Warari alisema. Warari alisema kengele hiyo ilikuwa imetengenezwa na shaba na ilikuwa ikitumiwa kuwakumbusha waumini saa za kuomba na pia kupanga ratiba ya kanisa hiyo.

Shamsa Ford Amchana Tena Rose Ndauka Kuimba Hujui Dada, Sauti Kama Umemeza Jiwe la Moto Kurap Muachie Rosa Ree

Ameandika Haya Shamsa ford Kumponda Rose Ndauka: Bora ukweli unaouma kuliko uongo unaokufurahisha. Nipige vijembe,kasirika lakini kuimba hujui dada .Yaani sauti kama umemeza jiwe la moto jamani .Ww baki kwenye bongo movie tu huko kwenye kuimba waachie kina Nandy,maua ,zuchu.Na hipop muachie Rosa Ree.Maana nyimbo yako hata hipop yenyewe imeshangaaNasikia umetoa nyimbo nyingine inaitwa SNITCH .Dada mkavu ww na press ukaita kuzindua nyimbo hata uoga .Poleni waandishi wa habari mnatubeba sana maana kuvumilia ile nyimbo inahitaji HEKIMA .Kwenye kikoba pia kumbuka mdogo wako anadaiwa si umlipie. mm na ww wote tuna njaa HABARI HIZI ZINAPATIKANA KWENYE APP YA

DJ Seven: Harmonize kwa sasa ndio msanii namba moja Tanzania, ndio wakati wake

DJ Seven: Harmonize kwa sasa ndio msanii namba moja Tanzania, ndio wakati wake Akiongea na @el mando tz DJ wa @harmonize tz @djsevenworldwide ameeleza kuwa watu wengi walikuwa hawaamini ukubwa wa Harmonize ila sasa wameanza kukubali, Harmonize ndio msanii pekee Tanznaia anayeweza kuandika wimbo kwa lugha mbili na ukapenbdwa kwa Kiingereza na Kiswahili. Sukari ya @officialzuchu ni ngoma kali sana hata Jeje ya @diamondplatnumz lakini pia kuna baadhi ya ngoma kwenye Album ya @mbosso , sisikilizagi nyimbo za @rayvanny ukijataja msanii namba moja kwa sasa Tanznaia ni Harmonize.  Tazama Hapa Chini Msanii Rosa Ree Akimkemea Shetani:   DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL => HAPA KUPATA HIZI HABARI KWENYE SIMU YAKO HATA BILA BUNDLE

© 2025 Vimarsana

vimarsana © 2020. All Rights Reserved.