Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Misri mjini Cairo, inaeleza kwamba Rais el-Sisi na Sullivan walizungumzia pia suala la ujenzi wa Ukanda wa Gaza, mvutano kuhusu bwawa la Ethiopia kwenye mto wa Blue Nile Gerd uhusiano kati ya Marekani na Misri na hali nchini Tunisia Yemen na Iraq.
Uchunguzi huo umegundua kwamba mkataba uliotolewa kwa kampuni ya Digital Vibes haukuwa sahihi na maafisa wa juu wamefaidika kutokana na baadhi ya pesa zilizolipwa na kampuni hiyo.
Serikali ya Tanzania Jumapili imesimamisha uchapishaji wa gazeti moja la kibinafsi kwa siku 30, baada ya kumhusisha mtu mwenye silaha, aliyetajwa na maafisa wa usalama kama“gaidi” ambaye aliua watu wanne, na chama tawala cha nchi hiyo.
Serikali iko katika shinikizo la kufungua tena shule, kwanza, kwa sababu za kielimu, lakini pia ikizingatia madhara ya kiuchumi ya kufunga shule za wamiliki binafsi ambao wanakabiliwa na hatari ya mali zao kuuzwa ili waweze kulipa mikopo ya benki, limeandika gazeti la The East African, Jumapili.
Mapema Jumapili, Idara hiyo imeeleza kuwa Ida “kimeendelea kuongezeka kasi kwa haraka” na kilikuwa kinaenda kwa upepo wenye nguvu ya juu kabisa wa kilomita 215 kwa saa.