Euro 2020: Italia yauwa ndoto za England Wembley | Michezo | DW
Euro 2020: Italia yauwa ndoto za England Wembley Baada ya kipindi cha karibu mwezi mmoja, mabao 145 ikiwa ni idadi kubwa zaidi ambayo tumewahi kushuhudia katika mashindano ya Ulaya, tamasha la euro 2020 limefikia tamati kwa Italia, kutwaa ubingwa Hadithi ya ukombozi wa kandanda la Italia imekamilika. Subira yenye uchungu ya nusu karne kwa England kushinda taji kubwa inaendelea. Na ni kwa sababu ya mikwaju ya penalti. Italia wameshinda Kombe la Ulaya – Euro 2020 kwa mara ya pili baada ya kuwafunga England 3 -2 kwa mikwaju ya penati jana usiku. Mechi ilimalizika 1-1 baada ya muda wa ziada dim...