Hatua ya Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria kufanyia tathmini sheria sita, ikiwamo ya uhujumu uchumi, imepokelewa kwa furaha na wadau wa sheria ikielezwa kuwa ni kilio cha muda mrefu cha kuondoa sheria kandamizi za muda mrefu.
Hatua hiyo imetangazwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi jana, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/2022, akisema lengo ni kufahamu kama sheria hizo zinaweza kutumika katika kupunguza msongamano magerezani.
Mbali na uhujumu uchumi, Profesa Kabudi alizitaja sheria nyingine zinazofanyiwa tathmini kuwa ni pamoja na Sheria ya Magereza, Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai na Sheria ya Huduma za Jamii, Sheria ya Bodi ya Msamaha na Sheria ya Kikomo cha Adhabu.
April 30, 2021
In total, Brazil has reported more than 14 million cases of COVID-19 and more than 400 000 deaths. Cases have now declined for four weeks in.
Baadhi ya Mali za Hotel ya Ngurdoto Zauzwa Kulipia Madeni ya Mishahara Milion 129
Baadhi ya Mali za Hotel ya Ngurdoto Zauzwa Kulipia Madeni ya Mishahara Milion 129
Baadhi ya mali za Hotel ya Kitalii ya Ngurdoto Mountain iliyopo Usa River, Wilayani Arumeru zimetakiwa kupigwa mnada ili kufidia mishahara ya watu 93 waliokuwa Wafanyakazi wa Hoteli ambao wanadai Tsh. Milioni 129
Amri hiyo imetolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Masijala Ndogo ya Kazi. Naibu Msajili wa Mahakama, John Nkwabi alitoa maamuzi hayo Aprili 26 ambapo kesi hiyo yenye namba 140 ya mwaka 2020, ilisajiliwa Oktoba 16 Mwaka 2020
Mali zitakazopigwa mnada ni vitanda 139, Gari aina ya Coaster yenye namba za usajili T847 DPH, kiwanja namba 418 kilichopo Block A eneo la Leganga, Usa River, na mashine nne za kufulia nguo
DC Hai Sabaya: akamata vifaa vya kutoa mimba na kung’oa meno ,alijifanya anafanya biashara ya mpesa
Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama imeongoza operesheni maalumu iliyofanikiwa kupatikana kwa vituo vya Afya Bubu ambavyo awali wamiliki waliendesha maduka yao kana kwamba wanafanyabiashara ya M-pesa/kubadili fedha kwa njia ya Mtandao huku kiuhalisia wanaendesha biashara ya kutibu na kuuza madawa ya binadamu kinyume cha kanuni na Taratibu za Afya.
Ole Sabaya ameelekeza mmiliki wa duka hilo Othaman Kimaro kushikiliwa na vyombo vya Dola ili atoe ushirikiano kwa matukio mbalimbali ikiwemo maelezo kuhusu vifaa maalum vya kutoa mimba, kung’oa meno, pamoja na kupatikana na madawa maalum ambayo kwa mujibu wa taratibu hutolewa kwa kibali maalum.
6 New FORM FOUR and Above Government Job Vacancies UTUMISHI at ATC, TUWASA and MNMA - Various Posts
6 New FORM FOUR and Above Government Job Vacancies UTUMISHI at ATC, TUWASA and MNMA - Various Posts