Floyd Mayweather Jr: Bondia anayeamini mwanaume anapaswa kuwa na wanawake wengi 27 Julai 2021, 06:59 EAT Chanzo cha picha, Getty Images Ni wanamichezo ambao uwezo,talanta na rekodi zao zitasalia katika kumbukumbu za historia kwa muda mrefu .Wengine wameshastaafu lakini wenzao bado wapo katika tasnia ya michezo.Wikii hii tunakupakulia safari za wanamichezo wa kipekee ambao wameng'ara na kuacha mifano ya kuigwa katika aina mbali mbali ya michezo.Leo tunamuangazia bondia Floyd Mayweather Jr Floyd Joy Mayweather Jr. amestaafu kutoka masumbwi na sasa anamiliki kampuni yake ya kusimamia mchezo h...